Na: Patrick Sanga
Waraka wa Novemba
Nakusalimu kwa jina la Yesu!
Biblia katika Ezekieli 33:7 inasema ‘Basi, wewe, mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi kwa nyumba ya Israeli, basi ulisikie neno hili kinywani mwangu, ukawape maonyo yangu’.
Ukisoma habari hii kuanzia ule mstari wa kwanza hadi ule wa tisa, utaona namna Mungu alivyosema na Ezekieli kuhusu wajibu wa ulinzi aliokuwa amepewa kwa watu wa Taifa lake. Jukumu lake kama Mlinzi ilikuwa ni kutoa taarifa kwa wale anaowalinda. Kila alipoona hatari alipaswa kutoa taarifa kwa wale anaowalinda. Kama mtu angekufa wakati mlinzi alitoa taarifa, damu yake, ilikuwa juu ya mtu huyo. Lakini kama akifa kwa kuwa mlinzi hukutoa taarifa basi damu yake ilidaiwa juu ya mlinzi husika. Naam jambo la msingi kujua ni kwamba kumbe mwanadamu amepewa kuwa mlinzi wa jambo fulani hapa dunaiani.
Isaya 62: 6-7 ‘Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Eee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha BWANA, msiwe na kimya; wala msimwache akae kimya, mpaka atakapoufanya imara Yerusalemu, na kuufanya kuwa sifa duniani’.
Naam maandiko haya yanazidi kudhihirisha na kufafanua kuhusu nafsi ya ulinzi kwa mwanadamu. Hapa Mungu alikuwa anasema na mji wa Yerusalemu kwamba ameweka walinzi juu ya kuta zake, na kazi yao ni kumkumbusha Bwana afanye kile alichoahidi kufanya juu ya mji huo kwa kutokunyamaza usiku wala mchana. Hii ina maana mfumo wa ulinzi wa Walinzi hawa wa kuta za Yerusalemu ulikuwa kwa njia ya kinywa kama ilivyokuwa kwa Ezeikeli pia. Kwa vinywa vyao walionya, waliomba, walifundisha nk. Naam Walinzi hawa walijua wajibu wao ni nini katika nafasi zao za maeneo yao ya ulinzi.
Ezekieli anatumbia kwa habari ya ‘mlinzi wa nyumba ya Israeli’ na Isaya anatuambia kwa habari ya ‘Walinzi wa kuta za Yerusalemu’. Tofauti hizi za ulinzi zinatujulisha kwa habari ya nafasi mbalimbali alizonazo mwanadamu katika ulimwengu wa roho.
‘Nyumba ya Israeli’ na ‘Kuta za Yerusalemu’ ni maeneo ya ulinzi, au maeneo yanayohitaji kulindwa na hivyo yanahitaji walinzi. Hata sasa yapo maeneo mbalimbali ambayo ni nyumba ya Israeli na kuta za Yerusalemu kwa jinsi ya rohoni, ambayo yanahitaji ulinzi wa kipekee ili makusudi ya Mungu yaweze kufanikiwa. Fahamu kwamba ‘kufanikiwa kwa kusudi la Mungu duniani kunategemea utiifu wa ‘walinzi’ wake duniani kwenye nafasi ambazo amewapa katika ulimwengu wa roho’. Huu ni mwanzo wa somo hili pana, endelea kufuatilia mfululizo wa somo hili ili upate kujifunza kwa namna gani ‘mwanadamu umepewa kuwa mlinzi’ kwenye maeneo mbalimbali ya maisha yako, watu wako, mji wako na Taifa lako nk.
Mungu akubariki, tutaendelea na shemu ya pili…
Mungu hufanya kazi pamoja na wampendao katika kuwapatia mema wale wampendao. Kwa hiyo sisi ambao tumeokoka lazima Mungu afanye kazi na sisi katika eneo la sisi kuombea na kupatanisha maeneo mbalimbali.
LikeLiked by 1 person
Amina kaka Moses,na tufanye kazi yake maadam ni mchana, usiku waja asipoweza mtu kufanya jambo lolote.
LikeLike
These are impressive articles. Keep up the noble be successful.
Heart Healthy Diet
LikeLike
hongera kaka
LikeLike
Ahsante, tuzidi kuombeana
LikeLike
Mungu azidi kukufunulia yalio sirini zaidi kanisa lipone
LikeLike
Amen, ahsante tuzidi kuombeana.
LikeLike
Mungu akuzidishie ufahamu juu ya neno lake, na akubariki sana
LikeLike
Amen, tuzidi kuombeana.
LikeLike
Ameni, nawe mungu akubariki
LikeLike
NA MUNGU AKUKUTIA NGUVU KATIKA HUDUMA ZAKO ZA KUFUNDISHA NENO LA MUNGU.
LikeLike
Amen, ahsante ndugu, tuzidi kuombeana.
LikeLike
Asante sana mtumishi wa Mungu, na Mungu aliekupa kipaji hiki cha kufundisha nenolake akutie nguvu akutegemeze uwe salama. Nimefurahi sana kupata blog kama hii, nanitaendelea kujifunza hadi siku ya mwisho.
LikeLike
Ubarikiwe, tuzidi kuombeana.
LikeLike
Somo zuri nimebarikiwa naomba haya masomo niwennatumiwa kwenye imel yangu Mungu akubariki sana.
LikeLike
Ahsante, nashauri ji subscribe kwenye blog hii ili kila niwekapo masomo mapya yaje moja kwa moja kwenye email yako. Maana kuna nyakati nabanwa kiasi cha kushindwa kutumia wasomaji wote wanaotaka nitume kwenye email zao pia. Ubarikiwe.
LikeLike
ujumbe umenibariki sana,ubarikiwe mtumishi.
LikeLike
Ubalikiwe Kwel Kaka Umenifundisha.
LikeLike
Ahsante, tuzidi kuombeana
LikeLike
UBALIKIWE M2MISHI GOD BLESS YOU
LikeLike
AMEN MTUMISHI MUNGU AZIDI KUKUINUA NAMI NAPENDA UWE UNANITUMIA MASOMO YOTE.PIA YALE MASOMO YA NDOA YAMENISAIDIA SANA NA SASA NIMEKUWA MWALIMU KWA WENGINE JUU YA MWANAMKE KUSIMAMA KATIKA NAFASI MUNGU ALIZOMPA ASANTE.
LikeLike
Utukufu kwa Mungu wetu, ahsante zaidi kwa maombi yako, njia rahisi ya kupata masomo yangu ni wewe kuji – subscribe kwenye blog hii, kila mara niwekapo somo jipya litakufikia. Amina uwe na amani, endelea na huduma njema ya kuujenga mwili wa Kristo huko ulipo, jambo la msingi ni kuomba upako fresh kila usimamapo.
LikeLike
as ante kaka kwa mafundisho yako
LikeLike
Ubarikiwe!!
LikeLike
Ubarikiwe kwa mafundisho mazuri sana
LikeLike
Jicho la Mungu linachungulia kuona kama kuna mtu anayelia kwa ajili ya dhambi zinazotendwa na watu,
LikeLike