NAMNA YA KUSIKIA NA KUIELEWA SAUTI YA MUNGU ILI IKUSAIDE KATIKA KUFANYA MAAMUZI (Sehemu ya 1)

Na: Patrick Sanga

1

Salaam katika jina la Yesu Kristo na heri ya Pasaka mpenzi msomaji.

Je ni kweli Mungu anazungumza na mwanadamu hata sasa? Hili ni moja ya swali ambalo watu wengi wamekuwa wakijiuliza na kukosa majibu muafaka kwani baadhi yao hawaamini kwamba ni kawaida ya Mungu kuzungumza na wanadamu. Kama ilivyokuwa katika agano la kale, agano jipya, naam hata sasa, Mungu ni yeye yule jana na leo na hata milele. Hivyo ni kusudio la ujumbe huu kuongeza ufahamu wako ili uweze kujua ni kwa namna gani Mungu huzungumza na mwanadamu na kisha nini ufanye ili kumuelewa Mungu anapozungumza. Naam fuatana name sasa katika mfululizo huu…

Kwa nini Mungu azungumze/aseme na mwanadamu? – mtu anahitaji kusikia sauti ya Mungu ili; (a) aishi sawasawa na kusudi au mapenzi ya Mungu awapo hapa duniani      (b) kujenga na kudumisha mahusiano/mawasiliano mazuri kati yake na Mungu (c) kuona kama Mungu aonavyo na hivyo kutafsiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni (Rejea Zaburi 32:8, 1Samweli 3:1 na Isaya 55:8).

Mambo mhumu kujua kuhusu sauti ya Mungu

Yafuatayo ni baadhi ya mambo muhimu ya kukusaidia kuijua, kuisikia na kuielewa sauti ya Mungu, nawe hunabudi kuyafahamu na kuyatenda;

  • Jenga na kudumisha mahusiano mazuri na Roho Mtakatifu – Ni vizuri ukafahamu kwamba Roho Mtakatifu yupo duniani sasa akiliongoza kanisa katika kuyatenda mapenzi ya Mungu. Hivyo uwepo wa mahusiano mazuri kati yako na Roho Mtakatifu ndio ufunguo wa mawasilaino mazuri kati yako na Mungu. Biblia katika 1Wakorinto 2:10 inasema ‘Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu… vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu’. Andiko hili linatuonyesha nafasi ya Roho Mtakatifu katika kutusaidia kuisikia sauti ya Mungu. Hivyo jenga na kudumisha uhusiano wako na yeye, itakusaidia sana katika kiujua na kuisikia sauti ya Mungu.

Roho Mtakatifu

  • Ongeza ufahamu wa viashiria (signal) vya mawasiliano kati yako na Mungu                              Ufahamu wa viashiria (signal) za mawasiliano kati yako na Mungu ni wa lazima ili kusikia na kuielewa sauti ya Mungu. Zipo alama mbalimbali kwa kila mwamini ambazo Mungu hutumia katika kusema naye. Biblia katika 1Samweli 3:9 inasema   ‘… Enenda, kalale, itakauwa AKIKUITA, utasema, Nena, BWANA; kwa kuwa mtumishi wako anasikia…’ Jambo ninalotaka ulijue hapa ni kwamba Mungu ana njia nyingi za KUITA, naam anaweza kukuita kwa sauti itokayo kinywani pake au KWA NJIA KUKULETEA ALAMA/VIASHIRIA VYENYE KUKUFANYA UJUE MUNGU ANANIITA. Kama ilivyo kwa jinsi ya kibinadamu anayekuita si lazima aongee, anaweza kutumia alama za mikono au hata maandishi nk, kukuita. Katika kukuita kwa njia ya viashiria/alama Mungu anaweza kuleta nguvu/msisimuko/ubaridi/maumivu fulani kwenye sehemu ya mwili wako au huzuni moyoni mwako kama ishara/kiashiria cha uwepo wake juu yako na hivyo KUTAFUTA/KUTAKA USIKIVU WAKO ILI ASEME NAWE. Hivyo ni lazima uwe na ufahamu na utafute kujua kuhusu alama/namna ya kwako ambayo Mungu hutumia kutafuta usikivu wako.

 

  • Ni lazima ujue kutofautisha sauti ya Mungu na sauti nyingine                                                                           Hili ni muhimu sana kwako kulielewa ili usije ukaipuuza sauti ya Mungu kwa kudhani ni mawazo yako au ni ya Shetani au usije ukatekeleza jambo ukiamini kwamba Mungu amesema nawe kumbe Shetani ndiye alisema nawe. Katika             1 Samweli 3:7 imeandikwa ‘Basi Samweli alikuwa hamjui BWANA bado, na neno la BWANA lilikuwa bado halijafunuliwa kwake’. Andiko hili linatuonyesha makosa aliyofanya kijana Samweli katika kuielewa sauti ya Mungu akiichanganya na babu yake Kuhani Eli. Ni muhimu ukaelewa kwamba Mungu anaweza kusema na wewe hata kama uko katikati ya mkutano wa watu wenye kelele nyingi sana. Hii ni kwa sababu Mungu hatumii mdomo kusema nasi bali anatumia moyo wako kuzungumza. Moyo ndio kiungo muhimu cha mawasiliano kati ya mtu na Mungu.

2

Ukisoma katika Matendo ya Mitume 12:22 Biblia inasema ‘Watu wakapiga kelele, wakasema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya Mwanadamu’. Kauli hii ya watu ilikuja baada ya Mfalme Herode kuhutubia watu na kutoa maneno makuu. Watu waliamini kwamba ile ilikuwa sauti ya Mungu, kumbe sivyo na matokeo yake Herode alipigwa na Mungu akafa. Tahadhari, kuna wakati mtu/watu/watumishi wanaweza kunena mambo makubwa na watu wakadhani Mungu wa kweli anasema ndani yao, kumbe ni mungu wa dunia hii. Na ndio maana ni muhimu wewe binafsi uongeze ufahamu wako katika kuijua, kuisikia na kuielewa sauti ya Mungu, ili hata mwanadamu akinena unajua kwamba hili limetoka kwa Mungu wa kweli au vinginevyo.

Naam zipo sauti mbalimbali ambazo zote zinalenga kupambana/kuharibu kusudi la Mungu ndani ya mtu, zipo sauti za wanadamu (wazazi, walezi, mwenza wa ndoa, viongozi wa kiroho), ipo sauti ya Shetani kupitia majeshi ya pepo wabaya nk. Ni lazima mwanadamu amjue sana Mungu kiasi cha kuweza kutofautisha sauti hizi. Na namna pekee ya kutofautisha sauti hizi na ile ya Mungu ni kuwa na ufahamu mkubwa wa neno la Mungu kwani Mungu hawezi kukuagiza kutenda jambo lililo kinyume na neno lake.

Photo 3

Katika sehemu inayofuata nitakuonyesha mambo mengine kadhaa kujua na kuyaelewa kabla sijaanza sasa kuandika kuhusu njia ambazo Mungu hutumia kusema na wanadamu. Maombi yako ni muhimu sana.

Kwa mara nyingine heri ya Pasaka na amani ya Kristo iwe nawe. Tutaendelea na sehemu ya pili…

Utukufu na heshima vina wewe Yesu! Wastahili BWANA.

33 comments

  1. Bwana yesu asifiwe mtumishi wa MUNGU nashukuru sana kwa mafundisho yako mtumishi naona kimya uja post mafundisho na sisi tunakiu ya neno la MUNGU ubarikiwe.

    Like

    • Hakika mosi naomba rehema kwa Mungu na kwa wasomaji wengine wanaofuatilia kwa karibu masomo kama wewe, naam usiache kuniombea, kuanzia Mei 2016 nitaendelea kufanya posting ya masomo mapya.

      Like

  2. BWANA YESU ASIFIWE MTUMISHI WA MUNGU SANGA NAOMBA UMWOMBEE MUME WANGU ARUDI MOSHI ALIPATA UHAMISHO KWENDA TANGA NIKASHINDWA KWENDA NAYE KWA SABABU YA KAZI NA WATOTO SHULE NA KUSIMAMIA UJENZI WA NYUMBA YETU NAOMBA MUUJIZA WA MUNGU UMFUATE AMEN

    Like

Leave a comment