ROHO YA HEKIMA NA UFUNUO

1Na: Patrick Sanga

Salaam katika jina lake BWANA Yesu

Katika Waefeso 1:17 Biblia inasema ‘Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi ROHO YA HEKIMA NA YA UFUNUO KATIKA KUMJUA YEYE’. Hili moja ya maombi muhimu ambayo Mtume Paulo alifanya kwa jili ya Kanisa la Efeso. Kila nisomapo mstari huu nimekuwa nikijuliza sana ni kwa nini Mtume Paulo aliomba maombi haya kwa kanisa hili?.

Katika kutafakari na kuendelea kujifunza niligundua kwamba kulikuwa na sababu kubwa tatu ambazo zilimpelekea Mtume Paulo kuwaombea jambo hili, na kutokana na umuhimu wake hata kwa kanisa la sasa ndiyo maana nimeona ni vema nikaliandika hapa ili na wewe msomaji uweze kujifunza.

Zifuatazo ni sababu kadhaa zilizompelekea Mtume Paulo aliombee kanisa la Efeso roho ya hekima na ufunuo na kwa sababu hiyo zinatusaidia kujua umuhimu wake kwa kanisa la sasa pia;

Ili waweze kumjua Mungu zaidi (Waefeso 1:17)

Waefeso 1:11 ‘Na ndani yake sisi nasi tulifanywa urithi, huku tukichaguliwa tangu awali sawasawa na kusudi lake yeye, ambaye hufanya mambo yote kwa shauri la mapenzi yake’.

4

Kazi ya roho ya ufunuo ni kumfunua Mungu kwa kiwango ambacho bado hujakiona wala kukizoea ili kuboresha uhusiano wako na Mungu na kukufanya umaanishe katika kumpenda. Ndiyo, lengo ni kumfunua Mungu kwako, kutoka kwenye kona tofauti tofauti ili umjue zaidi ili hali kazi ya roho ya hekima ni kukupa ufahamu (maarifa), werevu na busara katika kufanya maamuzi sahihi kuhusu uhusiano wako na Mungu na maisha yako kwa ujumla. Katika ufunuo kuna mambo ambayo Mungu atayaleta kwako na yanahitaji hekima katika kuyafasiri, kuyanena na kutenda.

Naam bado hatumjui Mungu kwa kiwango kitupasacho kumjua na ndio maana tunahitaji roho ya ufunuo. Roho ya ufunuo inamuongoza mtu kujenga mahusaino binafsi na Mungu wake tokana na ufunuo aliopata.  Roho hii inatuleta kwenye ufahamu muhimu kuhusu ulimwengu wa roho na kwamba ni lazima tuanze kuishi maisha katika ulimwengu wa roho kuliko vile tunavyoishi katika ulimwengu wa mwili ili kumjua Mungu zaidi.

Ili kujua mambo ambayo Mungu amewaandalia (1Wakorinto 2:9-10)

Katika fungu hilo Biblia inasema hivi ‘Lakini, kama ilivyoandikwa, MAMBO AMBAYO JICHO HALIKUYAONA WALA SIKIO HALIKUYASIKIA, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao. LAKINI MUNGU AMETUFUNULIA SISI KWA ROHO. Maana Roho huchunguza yote, hata MAFUMBO ya Mungu’. Pia katika Waefeso 1:18 imeandikwa ‘MACHO YA MIOYO YENU YATIWE NURU MJUE tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo’

5

Mungu anataka watu wake wajue kwamba yeye anayo mawazo (Yeremia 29:11), mbalimbali ambayo amewaandalia watoto wake. Mawazo hayo yameunganishwa na kusudi la kuwepo kwao hapa duniani na hawana budi kuyajua, kuyapata na kuyatenda. Naam ili wafikie hapo sharti juu yao na ndani yao, wawe na roho ya hekima na ufunuo.

Kumbuka katika kila nyanja ya maisha iwe kazi, uchumi, biashara, familia, huduma, ndoa nk, yapo mambo ambayo ameyaandaa na anataka uyajue. Naam ni jukumu lako kuendelea kujenga na kuboresha mahusaino yako na Roho Mtakatifu yawe mazuri daima.

Ili kuujenga mwili wa Kristo ipasavyo

Katika 1Wakorinto 12:7 Biblia inasema ‘Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana’.  Ukiendelea Katika 1Wakorinto 12:20 imeandikwa ‘Na jicho haliwezi kuuambia mkono, sina haja na wewe; wala tena kichwa hakiwezi kuaimbia miguu; sina haja na ninyi’ na ule mstari wa 25 unasema ‘Ili kusiwe na faraka katika mwili, BALI VIUNGO VITUNZANE KILA KIUNGO NA MWENZIWE(1Wakorinto 12:25).

Hivyo roho ya ufunuo inatoa ufunuo ili kufaidiana, lengo ikiwa ni kuusaidia mwili wa Kristo kuimarika zaidi. Naam kumbuka ufunuo huu ni kwa sehemu kwa lengo la kulijenga kanisa, mwili wa Kristo. Katika 1Wakorinto 12:11 imeandikwa ‘Lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye’. Na tena Mtume Paulo anamalizia kwa kusema ‘Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake’ (1Wakorinto 12:27).

Naam hakuna mtu anayepewa karama zote, kila mmoja anapewa kwa SEHEMU kama KIUNGO ili kwa kushirikiana, MWILI wa Kristo ujengwe vema. Naam kila kiuingo lazima kihakikishe kina kuwa na ufanisi unaotakiwa, si kwa ajii yake, bali kuhakikisha mwili wa Kristo unajengwa ipasavyo, kupitia ufunuo/uwepo wa kile kiungo.

Kanisa lazima lifike mahali pa kuwa na uelewa kamili juu ya mwili wa Kristo unavyopaswa kutenda kazi kupitia ufunuo wa Roho Mtakatifu kwa kuwa ‘Mungu amevitia viungo kila kimoja katika mwili kama alivyotaka (1Wakorinto 12:18). Naam kila mshirika unayemuona NI KIUNGO CHA MWILI WA KRISTO KUPITA KARAMA, VIPAWA NA HUDUMA ALIZOPEWA kwa lengo la kuujenga mwili wa Kristo.  Roho ya hekima ikuongoze kutenda na kujua kwamba karama, huduma na vipawa ulivyonavyo ni kwa ajili ya kuujenga mwili wa kristo.

Naam hatupaswi kumdharau mtu yoyote kutokana na hali yake ya nje kwa jinsi ya kibinadamu maana yeye ni kiungo kinachostahili heshima zaidi (1 Wakorinto 12:22) Kazi ya Mchungaji na viongozi wa kanisa ni kufuatilia ili kujua Mungu ameweka/ametoa/amefunua kitu gani (karama/vipawa/huduma) juu ya wale wanaowaongoza ili kuviendeleza kwa lengo la kuujenga mwili wa Kristo.

3

Hivyo tokana na umuhimu wa roho ya hekima na ufunuo juu ya kanisa la Mungu na kwa mtu mmoja mmoja ni vizuri tukachukua au ukachukua hatua ya kuanza kumomba Mungu akujalie roho ya hekima na ufunuo wewe binafsi, familia yako, jamaa zako na kanisa kwa ujumla ili manufaa yake yawe dhahiri katika mwili wa Kristo ulimwenguni kote.

Roho ya hekima na ufunuo na iwe nanyi

Utukufu na heshima vina wewe Yesu, wastahili BWANA!

21 comments

  1. Asante sana mwalimu Patrick. Somo limekuja kwa wakati wake. Ninaamini kuwa sisi (kanisa) tukiyazingatia haya uliyotufundisha yaani tukaomba roho ya hekima na ufunuo na tupewapo tukatenda kwa uaminifu basi mwili wa Kristo hakika utajengeka. Na hapo ndipo tutakapotimiza lile agizo la Mungu kwetu katika Mathayo 6:33 kuwa tuutafute kwanza ufalme wa Mungu na haki yaki ili mengine yote tunayoyahitaji atupatie, tena kwa kipimo cha kuzidishiwa.

    Mungu wa mbinguni akubariki sana Patrick.

    Martha.

    Like

  2. Mtumishi P Sanga sasa nitajuaje kama MUNGU kanipa roho ya hekima na ufunuo maana napenda sana kutembea kwenye kusudi la MUNGU yaani ni raha sana eti!! kwa kuwa utakuwa una amani sana na unachokifanya. Nimwombaje MUNGU mimi anisikie?

    Like

    • Shalom Ndg. Yared, ahsante pia kwa kutenga muda wako wa kujifunza kupitia blogu hii.
      Ni dhahiri kwamba utendaji wa roho ya hekima na ufunuo ni wa kipekee sana kwa mwamini. Kama nilivyofafanua kwenye somo hili kwamba ‘Kazi ya roho ya ufunuo ni kumfunua Mungu kwa kiwango ambacho bado hujakiona wala kukizoea ili kuboresha uhusiano wako na Mungu na kukufanya umaanishe katika kumpenda. Ndiyo, lengo ni kumfunua Mungu kwako, kutoka kwenye kona tofauti tofauti ili umjue zaidi ili hali kazi ya roho ya hekima ni kukupa ufahamu (maarifa), werevu na busara katika kufanya maamuzi sahihi kuhusu uhusiano wako na Mungu na maisha yako kwa ujumla’.
      Ukirejea andiko la 1Wakorinto 2:9-10 ni dhahiri kwamba mtu anaweza kujua kwamba amepewa roho hii kwa njia zifuatazao (a) Mabadiliko ya matokeo ya uongozi wa Roho Mtakatifu ndani yake (Zaburi 32:8) (b) Ongezeko lake la ufahamu kuhusu Mungu (kumjua Mungu) na (c) mabadiliko yake kiufahamu na hususani katika kufanya maamuzi ambayo yapo sawasawa na mapenzi ya Mungu na mwisho (d) mabadiliko ya mtu husika katika kuwaza kwake na kuomba kwake, hii ikimaanisha suala si tu kuomba bali kuomba kwa ufuno wa Roho Mtakatifu.
      Pengine kitu cha msingi ni kwamba, ili roho hii ifanye kazi ipasavyo na matokeo yake kuwa dhahiri mwamini lazima azingatie kutunza utakatifu wake na hivyo kutompa Ibilisi nafasi ya kuharibu mahusiano ya mwamini na Mungu wake. Endapo mwamini akampa Ibilisi nafasi na hivyo kumuasi Mungu, basi afanye hima kutubu na kutengeneza uhusiano wake na Mungu.

      Like

  3. …ahsante mtumish na ubarikiwe…
    ….mafundisho yako ni mazuri na nmeyapenda..
    ..mimi ni mwanafunzi wa chuo lakini pia tunamiliki blog ya kikundi…je naweza kuwa nacopy baadhi ya mafundisho yako na kuyaweka kwenye blog yetu kwa faida ya wengine ?.
    ..nitafurahi nikikubariwa…

    Like

    • Barikiwa sana Samwel, naam unaruhusiwa lakini kwa sharti kwamba yasibadilishwe chochote, yawekwe kama yalivyo, huduma njema. Naomba unitumie pia address ya blogu yenu.

      Like

    • Utukufu kwa Bwana Yesu, unaweza ndio, changamoto kwangu ni muda, njia rahisi ni kuji subscribe kwenye blog hii, punde niwekapo somo jipya litakuja kwenye email yako pia.

      Like

  4. Natamani mno kupokea mafundisho yoote yamhusuyo Roho Mtakatifu ili yanijenge kiroho , binafsi ninatapatapa kwa jinsi gani niweze kuupata neema hii ya Kujazwa na Roho Mtakatifu ! WhatsApp no yangu – 0693 551353 Mchungaji Daniel .

    Like

Leave a comment